Saturday, April 2, 2016

UBATIZO NI NINI?


MWONGOZO
“Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya  wa uzima. Kwa maana kama tulivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika  tutaunganika kwa mfano wa kuunganika naye; tukijua nano hili, ya kuwa utu wetu wa kale  ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena”. Rum 6:4-6... Soma zaidi.

Tuesday, March 29, 2016

HATIMAYE SIKU ZA IBADA KUBADILIKA

BADILIKO KATIKA UTUNZAJI WA SIKU YA SABA
 Mahali fulani katika zama za giza katikati ya siku zile za Kristo na siku zetu, utunzaji wa Sabato umebadilishwa kutoka siku ya saba ya juma kwenda siku ya kwanza.
Ni hakika ya kwamba amri ya Mungu inahusu kuitakasa na kuitunza siku ya saba kama Sabato. Hakuna uwezekano wowote wa kukosa kuelewa maana yake hapa. Amri ni hii:
"Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa." (Kutoka 20:8-11). .....Soma Zaidi.

Monday, March 28, 2016

UKIIFAHAMU KWELI ITAKUWEKA HURU

Mchungaji mmoja wa kanisa fulani alikuwa na huduma nzuri sana na maombi na maombezi kwenye local church yake. Si utaratibu wa kanisa lao kuwa na huduma ya maombezi. Kwa hyo akaanza kupangiwa mipango kuwa yuko kinyume na utaratibu wa kanisa. Askofu wake alivyokuja kuona huduma ile alifanyiwa mizengwe ya kufukuzwa kazi. Katika kujitetea akamwambia Askofu kosa langu liko wapi? Maana nimegundua katika maandiko watu wakiombewa kwa jina la Yesu wanapokea uponyaji, sasa kwanini kunizuia? .. Kusoma zaidi

Monday, January 5, 2015

VITA KWA NJIA YA MAOMBI

VITA KWA NJIA YA MAOMBI

"Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho" EFE 6:12.

Ndugu yangu, Paulo anatueleza jambo zito sana katika waraka wake huu. Paulo anatufundisha kubeba silaha zote za kupigana na adui ili tuweze kusimama kwa ushindi katika hivi vita. Pamoja na silaha zote anamalizia katika mstari wa kumi na nane kwa kusema kwamba "kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo ".!

Anatuambia kwamba kupigana kwetu huku ni kwa njia ya maombi! Kimahesabu, vita vyetu hivi tunavipiga kwa kutumia maombi. Vita hivi vya kiroho tunavipiga kwa kutumia maombi. Maombi ni silaha kubwa katika vita hivi. Ukiangalia silaha zote ambazo anazitaja
1. Kweli
2. Haki (Maisha safi yenye utii)
3. Utayari ktk huduma
4. Imani
5. Wokovu (Uhakika wa mahusiano ya mtu binafsi na Mungu)
6. Upanga wa Roho ambao Neno la Mungu.

Silaha kuu yenye kubeba silaha zote hivi ni maombi! "kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho".

Ndugu, kila siku unapaswa kukaa mkao wa kivita. Paulo anamuonyesha adui kama mtaalamu wa kupanga vita hivi. Ndo maana Paulo asema ktk mstari wa kumi na moja "Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani". Shetani ni mwenye hila kila wakati. Katika kazi zako ataweka hila, katika huduma yako ataweka hila. Katika kanisa lako ataweka hila. Katika uchumi wako ataweka hila. Kila kutaka kwako kumjua Mungu ataweka hila. Basi Paulo asema Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Basi acha kulala mtumishi. Simama tuvipige hivi vita. Kuna watu wanajiona hawana huduma katika kanisa. Huduma hii ya ukamanda wa maombi nafasi hii inakusubiri. Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Chukua hatua. Tumia mbinu zote za kivita vya kiroho tuweze kupambana na adui. 
Tuungane pamoja katika vita hii pia kwa ku-like page yetu tushirikiane katika kuvipiga vita hivi katika jina la Yesu na damu ya mwanakondoo.

Sunday, October 19, 2014

PRAY WITHOUT CEASING


“Pray without ceasing” (1 Thessalonians 5:17). How many times have we heard or recited this verse? Yet how often have we stopped to really ponder it? And how can we obey it?
Reading from JC Ryle’s “A Call to Prayer” has stopped me in my tracks and made me consider my own prayer life. It is a necessary evaluation for each of us:
“We live in days of abounding religious profession. There are more places of public worship now than there ever were before. There are more persons attending them than there ever were before. And yet in spite of all this public religion, I believe there is a vast neglect of private prayer. It is one of those private transactions between God and our souls which no eye sees, and therefore one which men are tempted to pass over and leave undone. I believe that thousands never utter a word of prayer at all. They eat. They drink. They rise…  but they never speak to God. They have not one word to say to Him in whose hand are their life and breath, and all things, and from whose mouth they must one day receive their everlasting sentence. How dreadful this seems; but if the secrets of men were only known, how common.”
“Unceasing, incessant prayer is essential to the vitality of your relationship to the Lord and your ability to function in the world,” writes John MacArthur in his book “Alone with God,” but what does “unceasing” prayer mean? MacArthur continues:

“To ‘pray without ceasing’ refers recurring prayer, not nonstop talking. Prayer is to be a way of life–you’re to be continually in an attitude of prayer. It is living in continual God-consciousness, where everything you see and experience becomes a kind of prayer, lived in deep awareness of and surrender to Him. It should be instant and intimate communication-not unlike that which we enjoy with our best friend.”