JE HIZI NI SIKU ZA MWISHO.?



Je, Hizi ni Siku Za Mwisho?

Nabii Daniel alizungumza juu ya “WAKATI WA MWISHO.” Mtume Petro alisema, “katika SIKU ZA MWISHO watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki.” Paulo alisema, “SIKU ZA MWISHO kutakuwako nyakati za hatari.” Wanafunzi wa Kristo walimwuliza juu ya “MWISHO WA ULIMWENGU.” Je, wakati huo umefika? Unaweza kuwa na uhakika?

Mpaka lini Kristo atarudi? Kabla tukio hili kubwa kuliko yote halijatokea, Biblia huongelea juu ya kipindi kinachoitwa “siku za mwisho ”— “wakati wa mwisho” —­ “mwisho wa ulimwengu [zama]”“mwisho wa mambo haya” — “mwisho wa siku” — na ya wakati ambapo historia ya mwanadamu, kama tuijuavyo, “itakapomalizika.”
Bila shaka, wengi wetu tunaojidai kuwa Wakristo hatuamini-amini katika tukio halisi la kurudi kwa Yesu Kristo duniani. Wengi tumekua tukijiuliza maswakli mengi ambayo yametufanya tuwe na shaka juu ya tukio hili ingawa tunaamini-amini kidogo yaani hatuna uhakka wa kutosha. Hii ni kutokana pia na hali halisi na mitazamo ya dunia hii.
Miongoni mwa wanaoamini, wengi wao huamini kwamba inaweza kutokea baada ya miaka mamia ijayo. Baadhi wanaamini inaweza kuwa “miaka maelfu ijayo.” Wengine kwa namna fulani wanafikiria juu ya “Har-Magedoni.” Wanahisi kwamba wakati unaweza kuwa mfupi lakini hawana uwezo wa namna ya KUJUA. Nataka leo nikuambie kwamba ufalme wa Mungu umekaribi, tena uko karibu mno… ndugu yangu hizi ni nyakati za mwisho…. Inatubidi kua tayari muda woote.

Hebu tuangalie mitazamo na uelewa wa watu mbalimbali.

Mitume wa Awali Walielewaje?
Mitume wa awali walifikiri kwamba Kristo angerudi wakati wa maisha yao. Paulo katika 1 Wakorintho 15:51 na 1 Wathesalonike 4:15, alipokuwa akiongelea ufufuo wa wafu utakaotokea Kristo anaporudi mara ya pili, alitumia neno “sisi” akitegemea kuwa mmoja wa wale ambao wangekuwa “hai, [tutakao] salia hata wakati wa kuja kwake Bwana.”
Katika waraka wake wa pili kwa Wathesalonike, Paulo alikuwa amegundua kwamba hapo awali alikuwa ameelewa vibaya muda wa kutokea matukio maalumu ambayo ni lazima yatangulie Kurudi kwa Kristo. Alienda mbele na kuonya dhidi ya wale ambao wangedanganya wengine juu ya lini tukio hili lingetokea.
Aliandika juu ya “kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo” na ndugu wanapaswa wawe waangalifu kwamba “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu”
(2 Wathesalonike 2:1, 3).

Je, unaweza kudanganyika? Hebu tuangalie Kurudi kwa Kristo Mara ya Pili

Je, tuko kwenye siku za mwisho? Kama ndivyo, unaweza kujua kwa hakika kwamba hii ni kweli? Yesu alisema kwa wanafunzi wake, Nitarudi tena(Yohana 14:3).
Siku arobaini baada ya kufufuka kwake, wanaume wawili (malaika) waliwaambia wanafunzi wake wakati anapaa mbinguni, “Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni”
 (Matendo 1:11).
Ndugu msimaji biblia inatuambia karibu ulimwengu utalifikia tukio la kurudi kwake kristo kama upeo wa juu kabisa. Tena, je, tunaweza kujua? Mathayo anaandika maneno ya Kristo: “Maana kama vile umeme uonekanavyo…ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu”  (Math. 24:27, 30, 37, 39, 42, 44, 46).
Usifanye kosa! Biblia iko wazi kuhusu Kurudi kwa Yesu Kristo. Mafungu mengi zaidi yanayoongelea Kurudi Kwake Mara ya Pili duniani yanaweza kunukuliwa. Kutatokea—na haitegemei juu ya mapendekezo ya wanadamu. Hata hivyo, kabla tukio hili la juu kabisa halijatokea, mambo mengine mengi zaidi yalisemwa yatatokea katika kipindi cha kuelekea matukio ya kutisha yanayotangulia kurudi kwake!
Dhana ya mwisho wa ulimwengu limekuwa ni somo lenye hisia, kejeli, mjadala, kusisimua na linalowafanya watu wafikiri kwa miaka 2,000. Bado, ni wachache wanaofahamu kiasi gani Biblia inaonyesha juu ya kile kinachoweza kueleweka kuhusu wakati huu.
“Siku na Saa”
Katika unabii maarufu wa Mlima wa Mizeituni kwenye Mathayo 24, wanafunzi walimwuliza Kristo, 3“Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja Kwako, na ya mwisho wa dunia?”.
(Mat 24: 3)
            Baada ya kujibu swali hili kwa kirefu, mafungu thelethini-na-tatu baadaye Kristo aliongeza katika fungu la 36 na kusema, 36“Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake”
(Mat 24: 36)
Je, hii inamaanisha kwamba hatuwezi kujua kiujumla wakati wa Kuja kwa Yesu Mara ya Pili?
Baadhi wanaamini hivi—na watu hawa hutupilia mbali hitaji lolote la kujishughulisha ili kujua lini kutakuwa Kurudi kwa Kristo.“Bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki”?
(Mathayo 24:50-51)
Ni wazi kwamba karibu kila mmoja hategemei Kurudi kwa Kristo Mara ya Pili katika wakati sahihi. Ukweli ni kwamba atarudi wakati ambapo wengi hawamtazamii kabisa. Kwa nini kuna wengi sana ambao hawawezi kutambua kuwasili kwa siku za mwisho?

Kitu gani kitawafanya wengi wasitambue mwanzo wa tukio hili kubwa?

Kristo alitoa mfano: “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.” Kristo alitamka kuwa tunaweza kujuamajira” ya Kurudi kwake Mara ya Pili,      
(Maat24: 32-33,)
Ndugu zangu tsiwe tayari kuridhika bila kujua kile ambacho Biblia inasema unaweza kujua!
Miaka mingi iliyopita, kulikuwa na usemi maarufu uliojulikana kama “Ishara za Nyakati. Niliufurahia na pengine nawe unaukumbuka. Kichwa hicho kilitolewa kwenye fungu lingine katika Mathayo. Kwenye sura ya 16, Mafarisayo na Masadukayo walimkabili Kristo, wakitaka “ishara” kutoka kwake. Aliwaita wanafiki, akisema, “Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa mbingu; lakini, je! Ishara za zamani hizi hamwezi kuzitambua?
Ingawa lengo la swali lao lilikuwa kutaka ishara kwamba Yesu alikuwa MASIHI (angalia Mathayo 12:38-40), mantiki ya Kristo ilikuwa kwamba hawakuweza kutambua matukio waliyokuwa wakiyashuhudia— “ishara za nyakati.”

Je, unaweza kutambua ishara za nyakazi ZETU?

Kristo aliwaambia wanafunzi wake, “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia” (Luka 21:28). “Mambo” ambayo aliyarejelea yanajumuisha mfululizo mzima wa matukio yaliyotabiriwa kutokea kwa mara ya kwanza katika historia! Mambo haya yanatokea—na yanazidi—sasa! Kuyatazama kwa haraka haraka hakutasaidia. Ni lazima tuchunguze kwa umakini ili kuweza kuzitambua “ishara za nyakati.”
Mungu amemtengea mwanadamu miaka 6,000 kujaribu serikali zake mwenyewe, falisafa, mifumo ya maadili, dini na miundo ya elimu. Fikira za kibinadamu hazitatui na hazina uwezo wa kumaliza matatizo makubwa ya ulimwengu. Miaka 6,000 ni kama imemalizika. Na, katika miaka 200 iliyopita au zaidi, ulimwengu umebadilika sana—na kwa haraka. Matukio yanatokea kwa haraka kwa namna ambayo haijawahi kuonekana huko nyuma!
Ulimwengu wa Karne ya Ishirini-na-moja
Kila mmoja anawafahamu watu fulani ambao huzunguka zunguka wakisimama kwenye mitaa wakipaaza sauti “Tubuni! Mwisho umekaribia!” Kikundi cha filamu cha Holywood kimewaigiza wengi kati yao. Bila shaka, hakuna mtu anayewajali sana watu kama hao. Lakini nyakati zimebadilika, na sauti zinazotuambia sasa kuwa mambo hayaendi sawa zimekuwa nyingi—tena mambo ni mabaya kabisa!
Wazo la kuwa na serikali moja ya dunia, lilibuniwa ili kuiokoa sayari na mwanadamu asijiangamize, linasikika mara nyingi zaidi. Hata hivyo, hakuna anayeonekana kujua namna ya kuunda serikali kama hiyo na kisha kupata ushirikiano wa kila mmoja ulio wa lazima ili kuifanya ifanikiwe!

Utazame ulimwengu unaokuzunguka. Unaona nini?

Ulimwengu mzima ulikuwa ni mahali imara mpaka mwanzoni mwa karne ya kumi-na-tisa. Katika wakati huo maendeleo ya viwanda yalizaa Zama Mpya. Haikuwahi kutokea mpaka takribani karne moja iliyopita ambapo watu walianza kuendesha magari na kuruka kwa ndege, na, tangu wakati huo, ustaarabu umekwenda kutoka “Zama za Nyukilia” hadi “Zama za Anga” na ndani ya muda mfupi chini ya nusu karne umefikia “Zama za Habari”.
Kuwasili kwa mavumbuzi mapya, kwa kasi kubwa katika historia, inabadilisha maisha kila siku. Hebu fikiria matokeo ya viwanda vya uchapaji na utaweza kukubali namna ambavyo uvumbuzi wa aina moja unavyoweza kuubadilisha ulimwengu. Kompyuta za kisasa zimefanya yayo hayo—na hakuna kurudi nyuma kwa sababu tu ya uvumbuzi huu mkubwa. Usafiri wa ndege uliwasili mwishoni mwa karne iliyopita. Japokuwa makadirio yanatofautiana lakini inasemekana kwamba maarifa ya mwanadamu yanaongezeka mara dufu kila baada ya miaka michache. Baadhi wanafikiri kuwa baada ya muda mfupi kasi itaserereka hadi kufikia kila baada ya miezi sita!
Mnamo mwanzoni mwa miaka ya 1970, Alvin Toffler aliandika kitabu kinachoitwa Fadhaa Ijayo (Future Shock). Kitabu hiki kikubwa kilielezea aina ya “bumbuwazi la kisaikolojia,” au madhara ya fadhaa, yatakayowapata watu kwa sababu ya kasi ya mabadiliko katika jamii. Toffler alidhihirisha kuwa mabadiliko haya yalianza kutokea miaka ya 1970 katika kiwango ambacho watu hawakuweza tena kuyatafakari.
Jamii ilianza kuingia kwenye kile ambacho Toffler alikielezea kama kuzidiwa—au “fadhaa.” Alielezea kwamba “yajayo” yalikuwa yanakuwa “yaliyopo” kwa haraka sana kiasi kwamba watu walianza “kutumia njia za mkato” namna ile ambayo ustaarabu ulikuwa haujawahi kuona. Miaka michache baadaye, aliandika kitabu kinachofutia kile cha kwanza kilichoitwa Wimbi la Tatu (The Third Wave). Kitabu hiki cha pili kilielezea kuongezeka kwa hali hii.
Picha aliyoielezea haikuwa nzuri, na sasa imekuwa mbaya zaidi!
Wakati “maendeleo” haya makubwa yakitokea, matatizo ya mwanadamu yamezidi kuwa makubwa au yasiyotatulika zaidi!
Makadirio ya ukubwa wa tatizo la UKIMWI yanapitiwa upya mara kwa mara na kuakisi mtazamo unaotisha zaidi kuliko ilivyofikiriwa hapo kabla. Sehemu nzima za wakazi wa Afrika zinakadiriwa kufutika kabisa ndani ya miaka michache kwa sababu tu ya ugonjwa huu mmoja. Lakini pia sio hilo tu bali pia na uwepo wa milipuko mbalimbali yamagomjwa ya kutisha kama vile EBOLA, MALARIA na mengineyo, yoote haya yakiiacha Africa katika hali mbaya sana.
Idadi ya watu duniani inayokadiriwa kuwa bilioni 6.9 (mapema 2009) inaongezeka kwa kiwango cha 1.2% kila mwaka. Hii ina maana kwamba kufikia mwaka 2050, idadi ya watu duniani itafikia bilioni 11.1! Makadirio haya yanakuja ingawa kuna ukweli kwamba magonjwa na njaa vinategemewa kuongezeka zaidi kwenye sehemu za dunia zinazokua kwa haraka sana! Kuzaliana kwa wingi katika nchi maskini duniani tayari kumeleta ongezeko hili la watu kama ilivyokadiriwa kutokea.

Sehemu ya Pili bonyeza HAPA

by Fortune akilimali.

No comments:

Post a Comment