KUZALIWA UPYA KIROHO

MAANA YA UBATIZO
“Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama kristo alivyofufuka  katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Kwa maana kama tulivyounganika naye katika mfan wa mauti yake, kadhalika tutaunganika kwa mfano wa kuunganika naye; tukijua nano hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena”. Rum 6:4-6.
Ubatizo huonyesha mambo muhumu matatu:-
Kuifia dhambi.
Kuzaliwa upya katika Kristo.
Kumpokea Kristo molele.
Ubatizo ni lazima uendane na imani ya kweli. Maana wote wenye imani ya kweli ni watoto wa Mungu,
1Yoh. 5:4. “Kwa maana kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huko ndiko kuushinda ulimwengu, hiyo imani yetu”.
Vivyo hivyo ubatizo huambatana na imani biblia inasema kuwa mtu ni lazima aamini ndio kasha abatizwe,  mtu hawezi kubatizwa ili hali hajui wala haamini kwa kile atakachokipokea…. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka” (Mk.16:16)
Hii ni sawa na kusema kuwa mtoto asijaribu kutembea mpaka awe na uhakika kuwa hatateleza na kuanguka .
Mambo muhimu kabla ya kubatizwa:-
Mtu huanza kwa kulisikia neno la Mungu; kwa maana  Imani huja kwa kusikia. (Rum 10:17)
Ni lazima kujifunza mambo unayopaswa kuyafanya ili kuikuza imani yake. Enendeni mkayafnye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza…… na kuwafundisha kuyashika yote  niliyoyaamuru mimi. (Mt.28:19,20).
Kasha fanya uamuzi sahihi wa kumfuata Kristo.
Ni lazima kupata toba na msamaha wa dhambi. “Tubuni mkabatizwe kila mtu kwa jina lake Yesu Kristo, mpate aondoleo ya dhambi.” (Mdo.2:38).
Mtu anapotaka kubatizwa ni lazima atubu ili kupata msamaha wa dhambi zake, na kuyaanza maisha mapya ya kiroho yenye uwepo wa Mungu, hii ni kwasababu uwepo wa Mungu hutoweka kabisa  palipo na dhambi. “Tubuni mkabatizwe kila mtu kwa jina lake Yesu Kristo, mpate aondoleo ya dhambi.” (Mdo.2:38)
Mtu anapotubu dhambi husamehewa kabisa na Mungu anasahau kabisa maisha ya awali ya mtu. “Tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.” (Mdo.3:19).
Mtu anapobatizwa mwili wake hugeuka hekalu la Mungu, yaani huitwa kuunganika kuwa mwili mmoja, “Ndiyo mlivyoitwa katika mwili mmoja”. (Kol.3:15).
Mwili huu mmoja unaozungumziwa ndilo kanisa, ambapo kichwa chake ni Kristo. “Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha Kanisa.” (Kol. 1:18)

No comments:

Post a Comment