MABADILIKO YA SIKU ZA IBADA SURA YA 3

SURA YA 3
KIBALI CHO CHOTE CHA UTAKATIFU WA JUMAPILI

JE KUNA KIBALI CHA MUNGU KWA BADILIKO HILI?
Kwanza kabisa inatupasa sote kufahamu kuwa maandiko ni neon la Mungu mwenyewe kama Biblia yenyewe inavyotuambia ya kwamba  iliandikwa  chini  ya  uvuvio  wake  Mungu,  na  kamwe  haijikanushi  yenyewe   “Kila andiko,  lenye  pumzi  ya  Mungu” (2 Timotheo 3:16).

Yesu Kristo hakubadili Sabato.  Yeye kama Muumbaji aliifanya ili iendelee kuwako.
“Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati [sheria] au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”                 (Mathayo 5:17).

KATIKA kipindi choote kabla na baada ya kristo, Wanafunzi wake Kristo na makanisa yale ya kwanza ya Kikristo hawakupata kusikia kitu kama hicho cha badiliko lililofanywa na Mungu kuhusu utunzaji wa Sabato.  Kwa hiyo,utunzaji wa siku nyingine yo yote kama Sabato mbali na ule wa siku ya saba hautambulikani katika Agano Jipya.

Ni dhahiri kwamba hakuna sehemu ndogo hata moja ya mahubiri Yake Kristo ambayo haionyeshi kitu gani ni halali na cha haki kutendwa katika siku ile ya saba, jambo ambalo ni gumu sana kulieleza kwa wale wanaodai kwamba wanasadiki [Kristo] aliitangua Sabato.

Ila kulikua na tofauti kati ya sharia za Sabato waliokua wakiishikilia wayahudi ambayo ilikua ni mzigo kwao na Sabato halisi ambayo Kristo alikua akiitunza. Utunzaji wa Sabato wa Wayahudi wa siku zile za Kristo ulikuwa haufanani kabisa na uleambao Mungu alikusudia.

Shetani alikuwa amefanya kila aliloweza kwa njia ya majaribu yake yapotoshayo kuwafanya. Wayahudi waache kuitunza Sabato. Katika jambo hilo alifanikiwa kwa sehemu tu.  Mungu akawaacha watu wake kwenda utumwani kule Babeli kwa sababu ya dhambi zao, ambazo zilikuwa ni pamoja na kuivunja Sabato. Mara tu waliporudi toka  utumwani, Wayahudi hao waliazimu kuitunza Sabato kwa uaminifu sana kama Mungu alivyoamuru kwa kuziweka sharia kali juu ya mtu yeyote atakayeivunja Sabato ambazo ziliwafanya wawe watumwa wa sheria.

Mbinu hii ya Siku ya Sabato kujazwa na masharti mengi yaliyokuwa mzigo mzito uliowalemea watu ilikua ni mbinu pekee ya shetani kuwafanya watu waendelee kuichukia siku hiyo ya Sabato.

Yesu alipojitokeza kama Mwalimu wa watu miongoni mwa Wayahudi, Alilitumia kila tukio kuiweka huru siku hiyo mbali na sheria zile zilizotungwa na wanadamu ambazo zilikuwa mzigo mzito uliowalemea watu.

MIUJIZA SIKU YA SABATO
Naam, alizitumia vizuri nafasi hizo, maana kwa makusudi mazima aliichagua Sabato kama siku ya kufanya miujiza Yake mingi pamoja na matendo yake ya huruma.

Akiwa ndani ya  sinagogi siku ile ya Sabato, alimtoa "roho ya pepo mchafu" kutoka ndani ya mtu yule aliyekuwa amefungwa na pepo huyo. Baadaye, Sabato ile ile, alimponya "homa kali" yule "[mkwewe Simoni], mamaye mkewe." (Angalia Luka 4:30-39.).

Hata hivyo, Yesu aliendelea tu kuyasahihisha mawazo yao kuhusu nini kilichofanya utunzaji wa Sabato uwe sahihi, naye aliendelea kufanya matengenezo katika utunzaji wa Sabato kwa kuwa "Mwana wa Adamu ndiye Bwana [Yehova] wa Sabato." (Mathayo 12:1-8.).

Vitabu vinne vya Injili huitaja siku ya kwanza ya juma mara sita, na katika mafungu hayo wale wanaoitunza siku ya kwanza ni lazima wakipate kibali chao kwa utunzaji kama huo. Vifungu vinavyoitaja siku ya kwanza katika Injili ni hivi:
a.      Mathayo 28:1
b.      Marko 16:1,2,9;
c.       Luka 23:56 na 24:1;
d.      Yohana 20:1,19.;

Ukivichunguza vifungu hivi kwa makini utagundua mambo yafuatayo:-
  1. Yanasema juu  ya Sabato, ni kweli, lakini  yanaainisha[yanatofautisha] kwa uangalifu mkubwa sana kati ya Sabato na siku ya kwanza ya juma, yakiliweka wazi jambo hili kwamba Sabato ya Agano J ipya ni siku ile iliyo kabla ya siku ya kwanza.
  1. Inadhihirika kwamba hayasemi kitu cho chote juu  ya badiliko la  Sabato.
  1. Hayatoi cheo [sifa] cho chote cha utakatifu kwa siku ile  ya kwanza.
  1. Yanatoa cheo [sifa] hicho kwa siku ile ya Saba.
  2. Hayasemi kwamba Kristo alistarehe siku ile ya kwanza, jambo ambalo lingekuwa la lazima katika kuifanya siku hiyo kuwa Sabato.
  3. Hayasemi lo lote kuhusu baraka yo yote kuwekwa juu ya siku ile ya kwanza.
  4. Hayatuambii lo lote juu ya Kristo kwamba kuna wakati wo wote aliopata kusema neno lo lote kuhusu siku ya kwanza, aidha kama ni siku takatifu, au vinginevyo.
  1. Hayatoi kanuni au amri yo yote kuhusu utunzaji wake [siku ya kwanza].
  1. Hakuna cho chote katika mafungu haya kinachotangaza kuwa siku ya kwanza iangaliwe na wafuasi wake Kristo kama kitu cho chote kile zaidi tu ya kuwa ni siku ya juma ya kawaida kama inavyotajwa ----- ni "siku ya kwanza ya juma" tu.

Mungu anasema kwamba Sabato ni “agano la milele” na ya kwamba ni “ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele”   (Kutoka 31:16,17).

Jiulize ndugu yangu ni nani aliyeipa cheo na mamlaka ya kuheshimiwa na amri ya kutuzwa siku hiyo ya kwanza?

Endelea kufuatilia makala hizi utaona ni jinsi gani, wakati gani, na nani aliyebadili majira haya na amri juu ya Sabato ya Bwana.

JE! KUNA VITABU VINGINE KATIKA BIBLIA VINAVYOONYESHA KUTAJWA KWA SIKU YA KWANZA NA KUTOA KIBALI CHA KUABUDU KATIKA SIKU HIYO?
KUTAJWA KWA SIKU YA KWANZA KATIAKA VITABU VINGINE VYA BIBLIA

Baada ya kuyatafakari kikamilifu mafungu yote haya, Kamusi ya Biblia iliyoandikwa na Smith, katika makala yake juu ya "Siku ya Bwana," anakiri kama ifuatavyo:

LICHA ya vitabu vya injili Siku ya kwanza ya juma imetajwa katika sehemu nyingine. Ya kwanza kati ya hizo imo katika kitabu cha Matendo ya Mitume:
"Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane. Palikuwa na taa nyingi katika orofa ile tulipokuwa tumekusanyika" (Mdo 20:7,8).

Kifungu hiki hakina ushahidi wo wote kuhusu badiliko la Sabato, wala hakiungi mkono wazo la utakatifu wa siku ya Jumapili. Ulikuwa ni mkutano uliofanyika siku ya kwanza ya juma, lakini sio mkutano wa ibada ya kawaida ya siku ya Jumapili.  Ulifanyika usiku. "Palikuwa na taa nyingi," na Paulo "akafuliza maneno yake hata usiku wa manane."

KABLA ya kuendelea kukichambua kifungu hiki, ni lazima kuchunguza katika biblia NI WAKATI GANI SIKU HUANZA na NI WAKATI GANI SIKU HUISHA.
Siku za Biblia zinaanza na kuisha jua linapozama [machweo].  Siku ya kwanza ya Biblia huanza jua linapokuchwa [machweo] Jumamosi jioni, na inakwisha jua linapokuchwa Jumapili jioni.  Kwa hiyo, "usiku wa manane" ambao Paulo  "alifuliza maneno yake" ni lazima ungekuwa, ungaliweza tu kuwa, ni ule wa Jumamosi usiku.

Ni dhahiri kuwa Mtume Paulo kama aligeuza siku hii na kuifanya jumapili siku ya ibada angekua ameivuna sharia ya Mungu,  “Dhambi ni uvunjaji wa Sheria  [Amri Kumi]”
(1 Yohana 3:4)
Hebu turejee vitabu vifuatavyo:-
Conybeare na Howson, katika kitabu chao cha 'LIFEAND EPISTLES OF THE APOSTLE PAUL,' wakishughulika na suala la wakati mkutano huo ulipofanyika, wanasema maneno haya:
"Ilikuwa ni jioni ile iliyokuja baada ya Sabato ya Wayahudi. Jumapili asubuhi merikebu ilikuwa tayari kwa safari." -----  (Scribner's ed., Vol.II, uk.206.) Daktari [Dkt.] Horatio B. Hackett, profesa wa Agano Jipya la Kiyunani [Kigiriki] katika Chuo cha Thiolojia cha Rochester, katika kitabu chake cha 'COMMENTARY ON ACTS,' asema hivi:

"Wayahudi walihesabu siku zao toka jioni hata asubuhi, na kwa kanuni ile usiku ule wa siku ya kwanza ya juma ungekuwa sawa na usiku wetu wa Jumamosi. Endapo Luka alihesabu hivyo hapa, kama wengi wanaotoa ufafanuzi wao wanavyodhani, basi, mtume alingoja mpaka Sabato ya Wayahudi ilipokwisha, na kufanya mkutano wake wa kidini wa mwisho [wa kuagana] pamoja na ndugu zake kule Troa... Jumamosi usiku, naye hatimaye aliendelea na safari yake
Jumapili asubuhi." ----- (Toleo la l882, uk.22l,222.)

Ahsante Mungu akubariki.

No comments:

Post a Comment