HISTORIA YA MAISHA YA KIKRISTO SEHEMU YA NNE

BAADA YA ANGUKO LA BABELI

Wakaijenga Babeli ikwa mji mkubwa, watu wote wakiwa na lugha moja. ”Wakasema, haya na tuujenge mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.”  (Mwa 11:4)

Baada ya babeli kuanguka, kilamtu alitoka Babeli akiwa na tamaduni za kipagani kuelekea suhemu mbalimbali za dunia.”8Basi BWANA akawatawanya waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.  9Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo BWANA alipochafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko BWANA akawatawanya waende usoni pa nchi yote.”  (Mwa 11:8,9)

Wakaondoka na ibada zao za kipagani kilammoja kwa lugha yake wakatawanyika kuelekea sehemu mbalimbali ya uso wa dunia, ibada ya mama na mtoto ikaendelea kuenea kama desturi yao,

Sanamu ya mama na mtoto ilitambuliwa kwa majina tofauti tofauti kutokana na kutofautiana kwa lugha. Tamuzi alijulika kwa majina yafuatayo;-
Huko China, mungu mke alijulikana kama “Shingmo”
Ufaransa na nchi nyingine za Ulaya alijulikana kwa majina tofauti tofauti yakionekana kuwa na maana sawa.

Afrodaiti wa Ugiriki na Venasi wa Kirumi .

Uingereza Tamuzi alijulikana kwa jina “Ester”.
Neno eostarun katika Kijerumani ndiko lilikotoka neno la Kijerumani Ostern.

“Asitate” kwa Wagiriki,
“Ashtorethi” kwa Wayahudi.
Huko Efeso mungu mke alijulikana kama “ARTEMI”, 
”Kwa maana mmewaleta watu hawa, wasioiba vitu vya hekalu wala kumtukana mungu mke wetu” (Mdo 19:37).

Ashtorethi -MALKIA WA MBINGUNI.
Mwanahistoria anayejulikana sana, Will Durant, katika kazi yake maarufu na yenye kuheshimiwa, Simulizi ya Ustaarabu, ku. 235, 244-245, ameandika, “Ishita [Asitate kwa Wagiriki, Ashtorethi kwa Wayahudi], hutuvutia si tu kwa sababu ni sawa na Isisi wa Kimisri na mfano wa Afrodaiti wa Ugiriki na Venasi wa Kirumi, bali kama mrithi halali wa moja ya tamaduni ngeni za Kibabeli…anajulikana kwetu hasa kutokana na ukurasa maarufu katika kitabu cha Herodotus: Kila mwanamke mzawa analazimika, mara moja katika maisha yake, kukaa katika hekalu la Venasi [Isita], na kufanya ngono na baadhi ya wageni.”

Je, ni ajabu kwamba Biblia huzungumzia mfumo wa kidini uliotokana na hilo jiji la kale kama, “SIRI, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI”    (Ufu. 17:5)?

“Watoto huokota kuni, na baba zao huwasha moto, na wanawake hukanda unga, ili kumfanyizia mikate malkia wa mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kinywaji, wapate kunikasirisha mimi.”  (Yeremia 7:18)

Mikate iliyokuwa inatolewa kwa malkia wa mbinguni ilikuwa ni haya haya maandazi ya moto yenye alama ya msalaba ambayo mamilioni ya watoto leo huimba juu yake (Alexander Hislop, Babeli Mbili, uk. 107). Kile kinachoonekana kutokuwa na hatia si safi hata kidogo.


Leo watu wanaweza kufikiri kwamba wanamwabudu Mwokozi wa kweli wakati kwa hakika wanaabudu mwokozi bandia—Yesu mwingine! Kwa hakika Ukristo wote wa kawaida unamwabudu Baali, mpatanishi na mungu jua, aliyeitwa jina kufuatia “mke” wake Ishita (ambaye kwa hakika alikuwa mama yake Semiramisi)—tutakuja kuona baadaye kuwa ndiye yule Biblia humwita “Malkia wa Mbinguni.”


“Malkia wa mbinguni” ni nani?
Ashtorethi—Malkia wa Mbinguni
Ibada ya Asitate (Isita) daima iliambatana na ibada ya Baali au kuabudu jua. Asitate alikuwa mke wa Baali. Angalia kwamba jina lingine la Asitate lilikuwa ni Ashtorethi. Nukuu ifuatayo inaliweka hili wazi. “Neno Isita lenyewe lina maana gani? Si jina la Kikristo. Linabeba asili yake ya Kikaldayo kwenye paji lake la uso. Isita halina maana nyingine zaidi ya Asitate, moja ya cheo cha Beltisi, malkia wa mbinguni…Sasa, mungu mke wa Waashuru, au Asitate, anatambulishwa kuwa ni Semiramisi na Athenagorasi (Legatio, kit. ii. uk. 179), na Lucian (De Dea Syria, kit. iii. uk. 382)…Sasa, hakuna jina ambalo lingeweza kuonyesha tabia halisi ya Semiramisi, kama malkia wa Babeli, zaidi ya jina la ‘Asht-tart,’ kwani hilo maana yake ni “Mwanamke aliyejenga minara”…Basi, Ashturit…ni wazi kwamba ndilo hilo hilo la Kiebrania ‘Ashtorethi’” (Alexander Hislop, Babeli Mbili, ku. 103, 307-308).
Angalia nukuu hii hitimishi kutoka Ensaiklopidia ya Microsoft Encarta Multimedia: “Ishita alikuwa Mama Mkuu, mungu mke wa uzazi na MALKIA WA MBINGUNI.” Hivyo, kiuhakika, Ashtorethi (Ishita) alikuwa mjane kahaba mama/mke wa Nimrodi, Semiramisi, kama wengi wa wanahistoria wa kale wanavyoshuhudia! Sasa Isita imewekwa imara kwamba si kitu kingine zaidi ya Ashtorethi wa Biblia! Sasa tunaweza kuchunguza maandiko yanayoonyesha jinsi Mungu anavyoitazama ibada ya huyu mungu mke wa kipagani—kwa jina lolote!
Mungu anaichukuliaje Isita?
Sasa kwa kuwa tunajua kuwa Isita ni mungu mke Ashtorethi, tunahitaji kutazama kwenye Biblia na kuona kile Mungu anachofikiria. Angalia fungu hili: “Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana...Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi [Isita]”                       (Amz. 2:11, 13).
Muktadha unaonyesha kwamba Mungu aliruhusu watu Wake wachukuliwe kutoka kwenye
nchi yao kwenda matekani kama matokeo ya dhambi hii! Huendelea, ikielezea jinsi ambavyo Mungu aliwakomboa watu Wake mara kwa mara tena kwa njia ya waamuzi. Baada ya kila ukombozi, Israeli aliwarudia miungu hao hao wa uongo, kitendo ambacho kilileta utekwaji nyara mara nyingine, kwa kushindwa na mataifa yaliyokuwa yakiwazunguka. Kamwe hawakuonekana kujifunza kama fungu la 19 linavyoweka wazi. “Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu… kwa kuifuata miungu mingine…na…hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi.” Katika sura ya 10 fungu la 6, Israeli anarudia mtindo huu wa ukaidi. Na Mungu, vivyo hivyo, bado hukiita kitendo hiki uovu.
Ibada za Baali na Ashtorethi zilijitokeza wakati wa Samweli. Samweli aliwaambia Israeli, “…iondoleeni mbali miungu migeni, nayo Maashtorethi yatoke kwenu, mkamtengenezee Bwana mioyo yenu, mkamtumikie yeye peke yake...Ndipo wana wa Israeli wakayaondoa Mabaali na Maashtorethi, wakamtumikia Bwana peke yake” (1 Sam. 7:3-4). Baadaye, katika 1 Samweli 12:10-11, Samweli aliielezea historia ya Israeli hadharani. Aliwakumbusha kwamba waliendelea kurejea katika kumtii Mungu, kisha kurudia ibada ya sanamu tena na tena!
Imesemwa kwamba “Kitu pekee ambacho mwanadamu amejifunza kutokana na historia ni kwamba hakuna mtu anayejifunza kutokana na historia.” George Santayana alienda mbele zaidi na kusema, “Wale wasiojifunza funzo la historia wana hatari ya kuirudia.”
Somo hili linawaelezea Israeli wa kale—lakini pia linaelezea ulimwengu mpya wa leo. Kwa sababu Isareli hawakudumu katika njia, hatimaye walitekwa mateka, wakapotea kutoka katika historia! Baada ya kutekwa nyara na kuadhibiwa mara moja zaidi, unabii unafunua kwamba Kristo atawakusanya kwa mara ya mwisho wakati wa Kurudi Kwake.
Mfano mwingine kutoka kwenye biblia.
Biblia husema kuwa Mfalme Sulemani alikuwa ndiye mtu mwenye hekima sana aliyewahi kuishi. Bado, alifanya kosa ambalo Mungu aliliona ni kubwa sana kiasi kwamba, baada ya kifo chake, Alimwadhibu Sulemani kwa kuuondoa ufalme kutoka kwa mtoto wake.
Kosa lake?
Alioa mwanamke aliyemwongoza katika kumwabudu Isita (Ashtorethi).
Angalia 1 Wafalme 11:4-6: “Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine...Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni…Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake.” Mafungu ya 11-12 yanaonyesha kwamba ufalme ulichukuliwa kutoka kwa mtoto wake.


Ibada ya sanamu ikiwemo desturi yao ya sala za kujirudiarudia ilisambaa na kuenea duniani kote, mfano mzuri was ala na namna hii zinaonekana huko Efeso. “Lakini walipotambua ya kuwa yeye ni myahudi, wakapiga kelele wote kwa pamoja kwa muda wa kama saa mbili wakisema, Artemi wa Waefeso ni mkuu”     (Mdo 19:34).
Mfumo huu wa sala ya kujurudiarudia ulionekana kushamiri sehemu mbalimbali katika uso wa dunia. Sheria kali ziliwekwa kwaajili ya mtu yeyote atakayepinga na kuidharau miungu yao.

Wakati mtume Paulo aliokua Assia akihubiri neon la Mungu walimshtaki na kumouna kuwa ni mtu anayekiuka maadili na kumdharau mungu wao mke Artemi. “Tena mnaona na kusikia ya kuwa si katika Efeso tu, bali katika Asia yote, Paulo huyo ameshawishi watu………. Si kwamba kazi hii yetu ina hatari ya kudharauliwa tu; bali hekalu la mungu mke aliye mkuu, Artemi , kuhesabiwa si kitu, na kuondolewa utukufu wake, ambaye Asia yote pia ulimwengu wote humwabudu”   Mdo(19:26).

Hili “kanisa mama” lina “mabinti madhehebu” wengi, na mfumo mzima hujificha chini ya bendera ya “Ukristo”, wakati kwa hakika ni “Dini ya Kisiri ya Kibabeli.” Biblia humwonyesha kama mdanganyifu wa watu wote pamoja na nchi zote za Kikristo zikiwa zimeleweshwa na mafundisho yake ya uongo! Anaonyeshwa kama aliyelewa kwa damu ya watakatifu, wakati huo huo, akijidai kwamba yeye ndiye kanisa la kweli. Mambinti zake wote wamerithi matendo yake ya kipagani.
Mamia ya mamilioni hutunza sikukuu ya ibada halisi ya miungu ya kipagani inayoitwa Isita, wakiamini kwamba wanamwadhimisha Yesu Kristo! Wengi hawajui kabisa kuhusu nini wanachokifanya. Jibu la Mungu kwa wote hawa ni “…zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu (Matendo 17:30)!
Lakini hebu tuone Yesu mwenewe anasemaje, Yesu aliwaambia Mafarisayo,“Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu”   (Math. 15:6, 9).
Maelezo sambamba ya Marko huongezea kitu cha muhimu:
Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu” (Mk. 7:9).

Kwa wazi mafungu haya yanawahusu wale wanaoikataa Pasaka ili wapate kutunza Isita ya kipagani.

No comments:

Post a Comment