MAANA YA UBATIZO

UBATIZO
Utangulizi
"Mtu YEYOTE akiyaongeza Mungu Atamwongezea hayomapigo yaliyoandikwa KATIKA kitabu HIKI Na MTU YEYOTE akiondoa lolote ktk Maneno ya UNABII wa kitabu HIKI Mungu atamwondolea sehemu KATIKA ULE mti wa uzima Na KATIKA ULE miji mtakatifu AMBAO habari zake zimeandikwa KATIKA kitabu hiki" Ufunuo 22:18b-1.

UBATIZO NI NINI??✍
"hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa KATIKA kristo Yesu tulibatizwa KATIKA mauti yake?. BASI TULIZIKWA PAMOJA NAYE KWA NJIA YA UBATIZO KATIKA MAUTI YAKE KUSUDI KAMA KRISTO ALIVYOFUFUKA KATIKA WAFU KWA NJIA YA UTUKUFU WA BABA  VIVYO HIVYO NA SISI TUENENDE KATIKA UPYA WA UZIMA. Warumi6:3-4
“Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya  wa uzima. Kwa maana kama tulivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika  tutaunganika kwa mfano wa kuunganika naye; tukijua nano hili, ya kuwa utu wetu wa kale  ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena”. Rum 6:4-6.

Kwa hiyo kubatizwa ni kuzika utu wa kale (Galatia3:27 )maana ninyi nyote mliobatizwa katika kristo mmemvaa kristo.
Ubatizo huonyesha mambo muhumu matatu:-
  1. Kuifia dhambi.
  2. Kuzaliwa upya katika Kristo.
  3. Kumpokea Kristo molele.
Ubatizo ni lazima uendane na imani ya kweli. Maana wote wenye imani ya kweli ni watoto wa Mungu,
1Yoh. 5:4. “Kwa maana kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huko ndiko kuushinda ulimwengu, hiyo imani yetu”.
Vivyo hivyo ubatizo huambatana na imani biblia inasema kuwa mtu ni lazima aamini ndio kasha abatizwe,  mtu hawezi kubatizwa ili hali hajui wala haamini kwa kile atakachokipokea…. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka” (Mk.16:16)
Hii ni sawa na kusema kuwa mtoto asijaribu kutembea mpaka awe na uhakika kuwa hatateleza na kuanguka .

MTU ANAYETAKIWA KUBATIZWA ANATAKIWA AWE  KAMA IFUATAVYO Aaminiye Na kubatizwa ataokoka asiye amini atahukumiwa..... marko16:15 ✍ NB:Kumbe anayetakiwa kubatizwa sharti aamini he hai wanaobatiza watoto wadogo wanakuwa wale watoto wamemwamini Yesu kristo awe bwana Na mwokozi wa Maisha Yao????
Neno la Kigiriki Babtiso ndio msingi wa neno ubatizo kiswahili baptism kingereza yaani babtiso zamisha zika funika kwa hiyo leo uwezi fanya Retsim nyunyiza unidanganye ndio ubatizo tuseme kweli tuache upotoshaji

Mambo muhimu kabla ya kubatizwa:-
  1. Mtu huanza kwa kulisikia neno la Mungu; kwa maana  Imani huja kwa kusikia. (Rum 10:17)
  1. Ni lazima kujifunza mambo unayopaswa kuyafanya ili kuikuza imani yake. Enendeni mkayafnye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza…… na kuwafundisha kuyashika yote  niliyoyaamuru mimi. (Mt.28:19,20).
  2. Kasha fanya uamuzi sahihi wa kumfuata Kristo.
  1. Ni lazima kupata toba na msamaha wa dhambi. “Tubuni mkabatizwe kila mtu kwa jina lake Yesu Kristo, mpate aondoleo ya dhambi.” (Mdo.2:38).

Mtu anapotaka kubatizwa ni lazima atubu ili kupata msamaha wa dhambi zake, na kuyaanza maisha mapya ya kiroho yenye uwepo wa Mungu, hii ni kwasababu uwepo wa Mungu hutoweka kabisa  palipo na dhambi. “Tubuni mkabatizwe kila mtu kwa jina lake Yesu Kristo, mpate aondoleo ya dhambi.” (Mdo.2:38)
Mtu anapotubu dhambi husamehewa kabisa na Mungu anasahau kabisa maisha ya awali ya mtu. “Tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.” (Mdo.3:19).
Utangulizi unasema atayeongeza...mapigo yanamngoja...
MAZINGIRA YA KUBATIZIA;
(Ubatizo wa Yesu "mathayo3:13 wakati huko Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka yordani kwa yohana ili abatizwe akabatizwa mstari 16""

Je nilazima tuende yordan kubatizwa???? (yohana3:22-23) baada ya hayo Yesu Na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya uyahudi akashinda huko pamoja nao, akabatiza. Yohana Nate alikuwa akabatiza huko Ainoni karibu Na salimu.
NB:Tunaona Yesu alibatiwa yordan lakini akaenda kuwabatiza watu huko nchi ya uyahudi Na Yohana alikuwa akabatiza huko ainoni kwa hiyo si LAZIMA  uende ukabatizwe yordani.

VIGEZO VYA SEHEMU YA KUBATIZIA
Yohana3:23 Yohana naye alikuwa akabatiza huko ainoni karibu Na salimu KWA SABABU KULIKUWA NA MAJI TELE NA WATU WAKAMWENDEA WAKABATIZWA  kwa hiyo sehemu ya kubatizia LAZIMA kuwe Na Maji tele siyo kwenye KIKOMBE AU BAKULIWADOGO,

SABABU YA KWANINI HATUBATIZI WATOTO WADOGO
Nitawajibu kuhusu watoto neno linasema watoto wenu hutakaswa na ninyi yaani wazazi,
Basis wakamletea watoto WADOGO ili awaguse . akawakumbatia akaweka mikono yake juu yao akawabarikia.. (Marko 10:13,16)
Kwa hiyo YESU mwenyewe hakubatiza watoto aliwabarikia tu kwa hiyo kuhani anawaombea Baraka.
NAOMBA SANA KILA ASOMAYE HUU UJUMBE AUANDIKE HATA KWENYE DAFTARI LAKE WAWEZA KUMSAIDIA SIKU NYINGINE.. HAPO NDIYO UJUWE WAPI WANAFUATA MAANDIKO NA WAPI WANABADILISHA MAANDIKO YALIVYOANDIKWA ASOMAYE NA ATAMBUE:

MAANA KIPOFU AKIONGOZWA NA KIPOFU MWENZIYE WOTE WATATUMBUKIA SHIMONI kwa watu hawasomi biblia Na hawataki kuokoka bwana wanasema wanamwamini Yesu halafu wanabaki huko kwenye DINI watabuluzwa hadi shimoni""
Mungu anatuonya 2Kor 6:14  "Msifungiwe NIRA pamoja Na wasioamini KWA jinsi isivyo sawasawa..... 17Basis tokeni kati yao mkatengwe nao ASEMA bwana siyo Mimi. Wewe umeijua kweli unang'ang'ania tu.
Yohana 8:31-32 Yesu akawaambia wale wayahudi waliomwaminii nanyi mkikaa KATIKA neno langu mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli. Tena mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru. Hero kulitendea neno kazi kuliko kuwa msikiaji.
NB:
Yesu alisema atakaye nionea haya Mbele za watu nami nitamwonea haya Mbele za Baba yangu Na Malaika zake. Napia akaesma wengi waatawachukieni si  ninyi bali kwa ajili ya Jina language kwa sababu mnaisema kweli..

Je, walioko jangwani ambapo hakuna mito wala ziwa neno linasemaje?

Yohana 3:3 “Yesu akamwambia, "Amen nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu." Moja ya maana ya ubatizo ni kuzaliwa upya.

Yesu anaposema kuzaliwa kwa maji na roho....anamaanisha baada ya tendo la kuzika dhambi kwa njia ya kufa na Kristo (baptiso)..na kufufuka pamoja naye..unapokea kipawa cha Roho Mtakatifu na unavikwa vazi la haki ya Yesu.
fungu 8 ni kudhihirisha matendo ya Roho Mtakatifu kwa mtu aliyemuamini Yesu na kubatizwa..Kazi za Roho hazichunguziki kwa macho isipokuwa katika vitendo.
Watoto hawawezi kuonesha tendo hata moja la Roho Mtakatifu kwa sababu hawajui neno lolote baina ya Wema na Uovu.

Wewe leo kwa kujitambua huwezi kujisaidia haja kubwa barabarani unajua si adili jema kwa sababu Roho ananena nawe...lkn mtoto hajui hilo.
Mtu anapobatizwa mwili wake hugeuka hekalu la Mungu, yaani huitwa kuunganika kuwa mwili mmoja, “Ndiyo mlivyoitwa katika mwili mmoja”. (Kol.3:15).

Barikiwa!.

No comments:

Post a Comment