HISTORIA YA MAISHA YA KIKRISTO SEHEMU YA TANO

KUENEA KWA DESTURI ZA KIBABELI ULIMWENGUNI KOTE

Ibada ya sanamu ikiwemo desturi yao ya sala za kujirudiarudia ilisambaa na kuenea duniani kote, mfano mzuri was ala na namna hii zinaonekana huko Efeso. “Lakini walipotambua ya kuwa yeye ni myahudi, wakapiga kelele wote kwa pamoja kwa muda wa kama saa mbili wakisema, Artemi wa Waefeso ni mkuu”     (Mdo 19:34).

Mfumo huu wa sala ya kujurudiarudia ulionekana kushamiri sehemu mbalimbali katika uso wa dunia. Sheria kali ziliwekwa kwaajili ya mtu yeyote atakayepinga na kuidharau miungu yao.

Ni dhahiri kwamba mfumo wa sala hizi uliambatana na shanga ambazo zilikua zikihesabiwa wakati wa sala zao za kiagani. Vilevle mfumo huu wa shanga unaonekana kushamiri pia katika nyakati hizi,

Huko india Wabudha wanatumia shanga zao ambazo zinayohesabiwa wakati wa sala, na mfumo was ala zao ni wa kujirudiarudia pia.

Waislamu nao wana tumia mfumo huu wa shanga iitwayoTashibi, inayohesabiwa wakati was ala zao za kujirudiarudia.

Halikadhalika Waroma nao wanatumia aina hii ya shanga/mkufu iitwayo Rozari, yenye pingili ‘55’ huhesabiwa pia wakati wa kusali na mfumo wa sala zao ni wa kujurudirudia.

Wakati wamisionari wanatembelea, nchi za kaskazini mwa dunia, ambako huko jua lilikua likichomoza maramoja kwa wiki, na kutokana na kwamba ibada hizi za kipagani zilikua zimekwisha kuenea, waliwakuta watu wakiabudu siiku ili jua lilipokua likionekana, kama ishara ya kumuenzi mungu jua,
Wamisionari walishindwa kubadilisha mfumo ule wa kuabudua na kwa sababu ilikua ni desturi yao kuabudu katika siku ile, ilibidi na wao waitumie siku ile kutoa mafundisho yao, siku hiyo ya kuabudu mungu jua ilijulikana kama “SUN  DAY”. Ambapo baadaye ikawa ndiyo siku iliyozoeleka na kuitwa “SUNDAY”.

Wamisionari hao walipofika pwani ya Afrka Mashariki, waliwakuta Waswahili wakivua na kula visamaki vidogo, Wamisionary hao walivipenda sana visamaki vidogo kwa kuwa vilifanana na moja ya miungu yao, mungu samaki aliyejulikana kama “DAGON”. Wakawa wanaviita DAG, DAG,DAG waswahili wa pwani ya Africa ya masharki wakaviita “Dagaa”.

Kama utakumbuka katika kitabu cha Samweli, wakati

2Wafilisi wakalichukua sanduku,la Mungu, wakalitia katika nyumba ya Dagoni, wakaliweka karibu na Dagoni.”     (1 Sam. 5:2.)

Moja ya miungu Wafilisti Waliokua wakiiabudu ni DAGON “mungu samaki” kama utaweza kufuatilia ni jinsi gani walivyokua wakimwabudu na kumpa utukufu mwingi wakidhani ya kuwa ndiye mungu wao Muumbaji.


Picha ya Dagon.

 


Hii ilitokea wakati Wafilisti walipoliteka Sanduku la Agano, nakwenda kuliweka kwenye nyumba ya DAGON, ilipofika subuhi ya siku ya pili, walishangaa sana kumkuta Dagon ameanguka kifudifudi, akilisujudia Sanduku la Agano la Mungu. Biblia inaeleza vizuri habari za Dagon katika kitabu cha Samweli wa kwanza.

Na watu wa Ashdodi walipoamka alfajiri siku ya pili, Kumbe! Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la bwana. Wakaitwaa Dagoni wakairudisha mahali pake tena.

Chakushangaza zaidi kwa watu hawa wa Ashdodi walipoamka tena asubuhi ya siku inayofuata wakamkuta tena mungu wao Dagoni amenguka kifudifudi mbele ya sanduku la Bwana, wakati huu hali ya Dagoni ilikua mbaya zaidi kwani alikua amevunjika kichwa na vitanga vya mikono yake, akabakia kiwiliwilwi tu.

4Hata walipoamka kesho yake asubuhi, Kumbe! Dagoni ameanguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA, na kichwa chake Dagon na vitanga vya mikono yake vyote viwili vimekatika, vipo vimelala kizingitini; Dagoni akasalia kiwiliwili chake tu. Kwa hiyo makuhani wa Dagoni na mtu awaye yote aingiaye nyumbani mwa Dagoni hawakanyagi kizingiti cha nyumbani mwa Dagoni huko Ashdodi, hata leo.”    (1 Sam. 5:4,5)


Matukio yoote haya yalikua ni kithibitisho cha kutosha kuwainesha wafilisti kuwa yuko Mungu mwenye nguvu kuliko yule mungu wao waliokua wakimtegemea na kudhani kuwa ndiye mwenyenguvu ambaye anaweza kuwasaidia.

Tunaona katika kitabu waamuzi jinsi Wafilisti walivyokua wakimtumainia mungu wao Dagon na kuamini kua hakika yeye ndiye alikua mweyenye nguvu kuliko miungu wengine

23Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui yetu mikononi mwetu. 24Na watu walipo mwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu”     ( Waamuzi 16:23-24)


UNABII WA DANIEL
Mungu anayefunua siri.
Baada ya dola ya Warumi  kuvunjika katika karne ya 5 B. K. Haikufuatiwa na dola nyingine yoyote kuu, na kwa kweli haijakuwapo dola ya tano ya kulinganishwa kimamlaka, pamoja na kuwepo jitihada kubwa za watu wenye tamaa kuunda nyingine.
Maeneo ya dola ya Kirumi yalimeguka kutokanana uvamizi wa makabila jeuri ya Kihan, Kigoti, Kivisigoti na Kivandali, yaliyoanzisha tawala zao wenyewe tofauti. Mataifa ya  sasa ya Ulaya yametokana na falme hizo. Katika kipindi chote cha historia ya miaka 1500 mpaka sasa, mataifa hayo yamebakia katika mgawanyiko, kama ilivyoashiriwa na nyayo za ile sanamu –nusu chuma na nusu udongo: “ nusu una nguvu, na nusu yake umevunjika … hawatashikamana.“
(Dan. 2:42-43)
KWA kuwa yupo Mungu anayefunua siri. Kama ilnsvyoelezwa katika kifungu hiki:-
“Yupo Mungu mbinguni afunuaye siri.. Mungu aliye mkuu amemjulisha mfalme mambo yatakayokuwa baadaye, na ndoto hii ni ya hakika, na tafsiri yake ni thabiti.” (Ms. 28,45)

Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akiwa amejaa kujikinai na ufahari, aliona katika ndoto sanamu moja kubwa sana  ya mtu, yenye sehemu tano (tazama uk. 16,17):
Kichwa cha sanamu kilikuwa cha dhahabu.
Kifua chake na mikono kilikuwa cha fedha.
Tumbo lake na mapaja lilikuwa la shaba.
Miguu yake miwili ilikuwa ya Chuma.
Lakini nyayo na vidole zilikuwa mchanganyiko wa chuma na udongo wa mfinyanzi.

Kisha jiwe likatokeza ‘lililokatwa kutoka mlimani bila kazi ya mikono.’ Likaangukia nyayo za sanamu ile, likaiangusha yote chini, na kuzisaga sehemu zake kuwa unga, kiasi kwamba upepo ukaupeperushia mbali. Baada ya hapa lile jiwe likakuakuwa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
Nebukadreza alisumbuliwa sana na hatima ya sanamu ile, kwa sababu hakuna kati ya watu wake wajuzi aliyeweza kumwambia ilikuwa na maana gani. lakini Daniel, nabii wa Israel alimwambia “kuna Mungu mbinguni afunuayesiri, naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayokuwa siku za mwisho      (Dan. 2:28).

Nabii  Daniel alielezea maana ya sanamu ile. “Kichwa cha dhahabu kiliwakilisha utawala wa Nebukadreza mwenyewe. Ulikuwa ufuatiwe na mwingine, wa hali ya chini zaidi (kifua na mikono ya fedha); na baada ya huo wa tatu (wa shaba); alafu wa nne (miguu ya chuma) ambao ungekuwa na nguvu na kishindo, lakini nyayo na vidole viliwakilisha falme zilizogawanyika, nusu nguvu na nusu dhaifu”.   (Ms. 37 –42)

NDOTO YA MAANA SANA
Wakati akitafakari mambo haya na akishangaa kama ufalme wake ungedumu milele, Nebukadneza alilala usingizi. Usiku ule alikuwa na ndoto ya maana, lakini alipoamka alikuwa hawezi kukumbuka kitu chochote. Alihisi hata hivyo, kuwa hii ndoto kwa namna fulani ilikuwa na majibu kwa swali lake juu ya mambo ya baadaye.

Mara moja Nebukadneza aliwaita wenye hekima katika utawala wake kumsaidia akumbuke ndoto yake haijalishi ni kiasi gani cha umizimu wao, unajimu, uchawi, au ulozi walihitaji kutumia. Wenye hekima walikusanywa, lakini hawakuweza, kupitia elimu ya mambo yote haya, kufunua ndoto ya mfalme.

 Akiwatambua hawa wenye hekima kuwa walikuwa wadanganyifu na kuwa wasingemsaidia, mfalme alikasirika na kuamuru wakamatwe na kuwekwa kizuizini wakisubiri kuuawa. Danieli na wenzake walidhaniwa kuwa wenye hekima, lakini hawakuitwa au kuwepo mbele ya mfalme. Hata hivyo, bado walijumuishwa katika kukamatwa wenye hekima kwa kijumla.

Danieli alikata rufaa ili hatua hii ya kuuawa icheleweshwe, akiahidi kuwa baada ya muda mfupi angempatia mfalme habari alizokuwa anazitaka. Usiku ule yeye pamoja na wenzake waliweka ombi lao kwa bidii mbele za Mungu ili kujua ndoto ya mfalme na tafsiri yake. Walijua kwamba Mungu huwaheshimu wale wanaoweka tumaini lao lote kwake, na kwa hiyo walienda kulala wakiamini kwamba Mungu angefanya mapenzi yake yatimie. Usiku ule Mungu kwa rehema alifunua ndoto ya mfalme kwa Danieli, na hali kadhalika ilichomaanisha, hivyo ikionyesha kwamba Mungu pekee anajua ya mbeleni.


SURA YA SANAMU YA FALME
Ndoto hii ya maana ilikuwa juu ya sanamu kubwa ambayo kichwa chake kilikuwa cha dhahabu. Kifua chake na mikono vilikuwa vya shaba. Miguu yake ilikuwa chuma, na nyayo zake na vidole vyake [pia] vilikuwa mchanganyiko wa chuma na udongo (angalia Danieli 2:28-33).

Kichwa cha dhahabu kilitafsiriwa wazi wazi kuwakilisha Babeli (angalia Danieli 2:37-38). Chini ya Nebukadneza, Babeli ilikuwa imekusanya dhahabu kutoka katika mataifa yote iliyoyateka, [dhahabu hii] ikiifanya kuwa taifa tajiri sana la zamani.

Lakini hiyo haiko katika ukuu wa utajiri unaodhaniwa, au katika hali ya kutoonekana ambayo mataifa au watu wanaweza kupata nguvu, bali katika kujua na kutimiza mapenzi ya Mungu. Na hatima yao inaamuriwa na mtizamo wao kwa makusudi ya Mungu kwao.

Ufalme wa Nebukadneza uliishia tu wakati wa utawala wa mjukuu wake Belshaza, wakati taifa la pili, lililowakilishwa kwa kifua na mikono ya shaba, lilipongia katika uwanja wa kutawala. Kwa ujumla, ni ufalme ulio hodari zaidi ambao unashinda ule ulio dhaifu, lakini unabii unaonyesha kwamba hii isingekuwa utaratibu wa mambo (angalia Danieli 2:39).

Katika sanamu, historia ya mataifa iliendelea kuanzia kwenye kichwa hadi kwenye miguu, na kila badiliko liliakisiwa kwa madini dhaifu yakilinganishwa na yale ya taifa lililotangulia.


BABELI YAANGUKA
Majeshi shirikisho ya Waamedi na Waajemi yaliushambulia na kuushinda ufalme wa Babeli, kumwua Belshaza--mfalme wa mwisho wa Babeli, na kisha Dario Mmedi alitawala katika sehemu yake (Angalia Danieli 5:28-31).

Zaidi ya karne moja kabla, Bwana alikuwa amefunua kupitia Isaya mbinu ambayo kwayo Babeli ingechukuliwa na mtu ambaye kupitia uongozi wake jambo hili lingetokea
(Angalia Isaya 44:27-28; 45:1-2).

Chini ya uongozi wa Koreshi Mwajemi, majeshi ya Waamedi na Waajemi, yaliweza kubadilisha mkondo wa maji ya Mto Frati kwa muda kidogo. Wakati wa kipindi hiki waliingia mjini kwa kutumia njia ya maji ambayo waliyakausha. Hata juhudi zao zisingekuwa na maana, kama malango ya shaba yasingekuwa yameachwa wazi, bila kulindwa na walinzi wanaotetea [ufalme], wakati mfalme na wakuu wake walisherekea na kunywa (Angalia Danieli 5).

Kama tu fedha ilivyo dhaifu kwa dhahabu kithamani, basi Waamedi--Waajemi walikuwa dhaifu kwa utajiri na anasa. Wakati Himaya ya Waamedi--Waajemi ilikuwa na nguvu katika mambo ya vita na eneo walilokalia, haikuweza kuizidi Babeli katika kujilimbikizia utajiri au elimu. Himaya ya Waamedi/Waajemi ilikuwepo kwa karibu miaka mia mbili, kuanzia 539 KK hadi 331 KK.

Ufalme uliofuata, ule wa shaba, ungewakilisha hatimaye ufalme ulioiangusha Uajemi. Tunajua kutokana na historia kwamba ilikuwa ni Wayunani, chini ya Alexander Mkuu, ambaye katika mapigano matatu ya nguvu (Granicus, mwaka 334 KK; Issus, mwaka 333 KK; na Arbela, mwaka 331 KK) aliyashinda majeshi ya Waajemi, akiifanya Uyunani Himaya ya baadaye.

Ukweli huu wa kihistoria unaonyeshwa pia waziwazi katika njozi nyingine na Danieli, ulioko kwenye kumbukumbu katika sura ya 8, ambapo inaelezwa ufalme wa kuwashinda Waajemi ungekuwa Uyunani (Angalia Danieli 8:2-8, 20-21).

Shaba yalikuwa ni madini yaliyotumiwa na Wayunani kote, na pia yaliletwa katika utengenezaji wa silaha na vyombo vya vita.

Roma, ambayo iliwakilishwa na miguu ya chuma, iliyashinda majeshi ya Kiyunani katika vita vya Pydna mwaka 168 KK. Roma hatimaye ilitawala ulimwengu kutoka mwaka 168 KK hadi 476 BK, wakati ilipoanguka mwishoni kwa makabila ya kivamizi ya washenzi.

Kwa zaidi ya miaka 500, Roma ilionekana kuwa isingeshindwa. Bendera zake zilipepea kutoka visiwa vya Uingereza mpaka mto Frati, Kutoka Bahari ya Kaskazini mpaka Jangwa la Sahara. Makaisari wake waliabudiwa kama miungu, na kwa uwezo wake ilifanya ulimwengu wote kama nyumba moja ya kifungo. Katika maneno ya mwanahistoria Edward Gibbon, “Kupinga ilikuwa ni hatari ya kifo, na isingewezekana kuruka.” The Decline and Fall of the Roman Empire, gombo la 1, ukr. 190.

Wakati Roma ilipoanguka, eneo lake liligawanywa katika sehemu kumi ambazo sasa zinafanya mataifa ya Ulaya. Kama ambavyo chuma na udongo kwa sehemu vina nguvu na kwa sehemu dhaifu, kwa hiyo ndivyo ingekuwa kwa mataifa haya kumi ya Ulaya ambayo nyayo na vidole vyake vya sanamu hii ilichowakilisha. Kama ambavyo chuma na udongo haviwezi kuchanganyika au kushikamana, kwa hiyo mataifa haya yenyewe yasingeungana kama dola ya mamlaka inayotawala ulimwengu.

Kwa karne kumi na tatu za mwisho, watu wenye nguvu wametafuta kuhuisha utukufu wa Himaya ya Kirumi ya zamani, wakiunganisha pamoja mataifa mbalimbali ya Ulaya. Tukianza na Charlemagne na kuendelea na Charles V, Louis XIV, Napoleon, Kaiser William II, na Adolph Hitler--wote kwa ishara wameshindwa, japo kwa wakati lengo lilionekana kufikiwa. Maneno saba madogo ya unabii yalisimama katika njia yao:

“Hawatashikamana, kama vile chuma kisivyoshikamana na udongo” Danieli 2:43. Na mataifa ya Ulaya, moja moja au yote, hayatashikamana katika mamlaka ya kutawala ulimwengu tena!


NDOTO BADO HAIJATIMIZWA
Lakini hii haikuwa mwisho wa ndoto. Pia ilifunuliwa kwamba katika siku za falme hizi, Mungu wa mbinguni atasimamisha Ufalme wake wa milele. Ufalme huu wa haki, uliowakilishwa na jiwe [mwamba] ambalo liligonga sanamu miguu yake, ungeendelea kukua mpaka dunia yote ijazwe, na hakuna hata mamlaka moja ya dunia ambayo ingezuia (Angalia Danieli 2:34-35, 44).

Ingawa wafalme wengi na mamlaka zimejaribu kumharibu Kristo--aliyewakilishwa na Jiwe, na wameendesha vita dhidi ya wafuasi wa ufalme wa Kristo wa haki, bado hakuna hata [ufalme mmoja] uliofanikiwa na wala hakuna utakaofanikiwa. (Angalia 1 Wakorintho 10:4)

Kristo na ufalme wake utatawala milele, utukufu wake na kweli utafunika na kuijaza dunia hii kama tu maji yaijazavyo bahari Na mataifa yote maovu ya dunia yatasagwasagwa kama unga wakati Kristo--Mwamba anapokuja tena katika mawingu ya mbinguni.


BADO KUNA MUDA WA KUANGUKA KWENYE JIWE
Rafiki, je utakuja kwa Kristo leo, ukianguka juu ya Mwamba huu wenye nguvu na kuvunjika katika moyo, ukitubu dhambi zako zote upate kuinuka na kuishi maisha mapya ukiwa na nafasi ya kuwa na uzima wa milele ikiwa utakuwa mwaminifu hadi mwisho?

Au utabaki na majivuno na kutotubu, uking’ang’ania kwenye dhambi zako utakapokuwa umechelewa, na kukutikana na Mwamba huu wa nguvu ukikuangukia na kukusaga mpaka kuwa vumbi--bila nafasi ya uzima wa milele?

Ndugu msomaji, je unataka kungukiwa na Mwamba huu mkuu na kupotea? Au unataka kupata hifadhi na kujificha katika Mwamba huu na kuokolewa? Uchaguzi ni wako.

“Ee Mungu, ukisikie kilio changu, Uyasikilize maombi yangu. Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda. Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, Ngome yenye nguvu adui asinipate.” (Zaburi 61:1-3.)



“Ingia ndani ya jabali; ukajifiche mavumbini mbele za utisho wa BWANA, mbele ya utukufu wa enzi yake.”
(Isaya 2:10.)


“Nimekukimbilia Wewe, BWANA, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye, uniopoe, Unitegee sikio lako, uniokoe. Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Nitakakokwenda siku zote. Umeamuru niokolewe, Ndiwe genge langu na ngome yangu.”
(Zaburi 71:1-3.)


“Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.”
(Yohana 6:37)



Ili kupata habari zaidi juu ya mada hii muhimu, tafadhali bonyeza hapa

No comments:

Post a Comment