UNABII NA MAANA YAKE

Unabii Ni Nini?
Unabii umefafanuliwa kuwa ufunuo wa matukio ya wakati ujao, hata kabla hayajatokea. Unabii wa kweli ni ujumbe ulioongozwa na roho ya Mungu, ambao umeandikwa au kusemwa, yaani, ufunuo kuhusu mapenzi na kusudi la Mungu. Katika Biblia kuna unabii mbalimbali kuhusu kutokea na kutambuliwa kwa Masihi, “umalizio wa mfumo wa mambo,” na pia ujumbe mbalimbali wa hukumu kutoka kwa Mungu.—Mathayo 24:3; Danieli 9:25.

Leo, watu wanaosemekana kuwa na hekima, yaani, wataalamu wa sayansi, uchumi, afya, siasa, mazingira, na taaluma nyinginezo, hujaribu kutabiri wakati ujao. Ingawa matabiri yao yanatangazwa sana kwenye vyombo vya habari na yanapendwa na watu wengi, matabiri hayo ni makisio tu yanayotegemea ujuzi au maoni fulani ya kibinafsi. Isitoshe, kwa kila utabiri unaotolewa, kunakuwa na matabiri mengine chungu nzima yenye kuupinga. Kwa kweli, ni jambo hatari kutabiri wakati ujao.
Chanzo cha Unabii wa Kweli

Hivyo, basi, ni nani aliye chanzo cha unabii wa kweli, na ni nani anayeweza kufasiri unabii huo? Mtume Petro aliandika: “Hakuna unabii wa Andiko unaotokana na fasiri yoyote ya kibinafsi.” (2 Petro 1:20) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “fasiri,” au “tafsiri,” linamaanisha “kusuluhisha au kufunua,” likionyesha kwamba “kinachofunguliwa kilikuwa kimefungwa.” Hivyo, Biblia fulani inatafsiri hivi maneno ya Petro: “Hakuna unabii wala Andiko linaloweza kufunguliwa na . . . mtu binafsi.”
IMANI NI NINI??
         Watu fulani hufafanua imani kuwa itikadi ya kidini katika Mungu bila uthibitisho thabiti wa kuwapo kwake. Mwandishi-habari Mmarekani H. L. Mencken alifafanua imani kuwa “itikadi isiyo ya kiakili ya mambo yasiyoelekea kutukia.” Je, hii ni imani ya kweli kama ifafanuliwavyo katika Biblia? Ni muhimu kuelewa imani waziwazi kwa sababu, kama ilivyonukuliwa juu, ‘bila imani haiwezekani kumpendeza Mungu.’Biblia husema: “Imani ni kuwa na hakika juu ya mambo tunayotumaini.” (Waebrania 11:1, The New Testament in the Language of Today) Kwa hiyo, imani hutegemea ujuzi sahihi, mambo hakika ambayo hutegemeza maamuzi yanayofaa. Imani haihusishi tu itikadi bali pia sababu ya kuitikadi.
Hakuna kitu kisichoeleweka zaidi kuliko wokovu. Kwa nini watu wengi wamechanganyikiwa—wamedanganyika—kuhusu kile watakachofanya baada ya maisha haya? Je, wokovu huja kwa neema au kwa njia ya matendo—na tofauti yake ni nini? Kwa namna gani—kwa vigezo vipi—watu hulipwa katika maisha yajayo? Kijitabu hiki cha muhimu sana kinaondoa mkanganyiko wote!
Kwa kielelezo: Labda una rafiki unayeweza kusema hivi juu yake: “Namtumaini mtu huyo. Ahadi zake zinategemeka. Najua kwamba niwapo na tatizo, atanisaidia.” Haielekei kwamba ungesema hivyo kuhusu mtu fulani uliyemjua kwa siku moja au mbili, sivyo? Angehitaji kuwa mtu ambaye amethibitika kuwa mwenye kutegemeka tena na tena. Ndivyo ilivyo na imani ya kidini, inayopaswa kutokeza tumaini na usadikisho unaotegemea uthibitisho wenye kutegemeka.
Mwinjilisti maarufu aliwahi kuulizwa mbinguni kutakuwa kwa namna gani. Alijibu, “Sijui lakini itakuwa ni ajabu na wote tutakuwepo pale.” Akakwepa swali.
Tanzia nyingi husema kuwa “waliofariki” “huenda nyumbani kuwa na Bwana.” Wengine huandika kwamba ndugu zao wapendwa waliofariki “waliungana na malaika” na kwamba “sasa hivi wanatuangalia.”
Baadhi wanaamini kwamba “wanaelekea kwenye utukufu.” Wanapoulizwa hii ina maana gani, wengi hawana uhakika. Lakini fikira za kawaida sana ni kwamba kila mmoja “atapaa mawinguni,” “kupiga vinubi,” “kutembea katika mitaa ya dhahabu mbele ya lango la lulu,” “kukaa katika viti vya kunesanesa” ama tu “kuzunguka mbinguni siku nzima.”
Mamia ya mamilioni wengine wamefundishwa kuamini kwamba wokovu ni kuutazama uso wa Yesu milele. Si tu kwamba wazo hili limejengwa katika uelewa potofu wa maandiko, lakini pia linafundisha kwamba hakuna atakayeweza kuuona uso wake moja kwa moja.

Ni kitu gani kinaweza kuwa cha kuchosha zaidi ya kutimiza mojawapo ya fikira hizi? Sitamani kufanya lolote la mambo haya kwa muda kitambo—achilia mbali kwa MILELE YOTE! Mtu fulani alipotafakari juu ya fikira hizi, alipendekeza kwamba ni “bora akaenda ahera, kwa sababu huko kunaonekana kuvutia zaidi.”
Mkanganyiko mwingi ajabu! Ujinga mwingi sana! Walio wengi wamedanganywa katika kuamini wokovu wa uongo.
Ni kitu gani umekisadiki bila kukithibitisha? Ni fikira gani maarufu uliyoifyonza bila kuchunguza ili kuona kile ambacho hasa Biblia hufundisha?

1 comment: