HISTORIA YA MAISHA YA KIKRISTO SEHEMU YA KWANZA



SEHEMU YA KWANZA
WAKRISTO WA AWALI KABLA YA GHARIKA
Zamani wakati wafuasi wa Kristo wakiieneza Injili ya Yesu Kristo, wapagani waliona kuwa, adui dhidi ya Mkombozi angedhihirishwa kwa wote ambao wangeliamini jina lake.

mbali: kwa hiyo, moto wa mateso dhidi ya wakristo iliwashwa. Ghafla wakristo wakanyanganywa mali zao na kuondolewa katka nyumba zao. Watu wingi; waungwana na watumwa; matajiri kwa masikini; wenye elimu na wasio na elimu, wakauawa bila Upagani uliona kuwa kama Injili ingeshinda,mahekalu na madhabahu yake yangefutiliwa huruma.

Hapo ndipo walipoyakumbuka maeno ya Yesu Kristo aliyowaeleza wanafunzi wake,”9Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakua watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu  21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitauwapo kamwe.”(Mat.24:9,21).

Tangu wakati wa nero mateso yaliendelea kwa karne kadhaa, wakristo walisingiziwa kuwa vyanzo vya njaa  maafa na matetemeko. Watoa habari walikua tayari kulipwa ili kutetea udanganyifu kua wakristo ni waovu.

Wakristo walizidi kuvumilia na kuendelea kuitetea imani yao, wakiyakumbuka maneno ya Yesu na ahadi zake kwa watakaokua washindi; lakini wakijua kuwa sikuhizo ni chache na zimekwisha fupizwa kwa ajili ya wateule..”Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeliokoka mtu yeyote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo”.(Mat.24:22).

Lakini pia maneno ya Yesu yalizidi kuwatia nguvu wakijua ya kuwa tuzo yao ni kubwa mbinguni, kwani ndivyo manabii walivyoteswa kabla yao.”11Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neon baya kwa oungo, kwa ajili yangu12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni”(Mat 5:11,12).

Kwa imani walimwona kristo na malika wakiwaangalia kwa shauku kubwa na kuheshimu uthabiti waona kuukubali. Sauti ilikuja kutoka katika kiti cha enzi cha Mungu10Uwe mwamnifu hata kufa, name nitakupa taji ya uzima.”(Uf.2:10)

Juhudi za shetani za kuangamiza kanisa la Mungu kwa vurugu hazikusaidia. Watendakazi wa Mungu waliuawa na injili ilizidikuenea na wafuasi wa kristo walizidi kuongezeka mara dufu, mkristo mmoja alisema “Kadiri mnavyotufyeka, ndivyo tunavyoongezeka; damu ya Wakristo ni mbegu

Mipango ya shetani ya kupambana na Mungu kwa ufanisi iliwekwa kwa kupandisha bendera zake katika kanisa la Wakristo ili akipate kile alichokikosa, mateso yakakoma. Badala yake kukawa na vishawishi vya mafanikio na heshima ya kidunia
Waabudu sanamu walipewa kupokea sehemu ya imani ya Kikristo. Walidai kuwa wamempokea Kristo lakini walikua hawjashawishikaa kuwa ni wenye dhambi, na hawakua hawajaona haja ya toba wala badiliko la moyo.
Uongo dhidi ya ukweli uliendelea na mpango wa shetani wa kuwayumbisha na kuwapoteza wana wa Mungu uliendelea kama ilivyoonyeshwa kwenye sura inayofuata.



No comments:

Post a Comment