HISTOTIA YA MAISHA YA KIKRISTO SEHEMU YA PILI


BAADA YA GARIKA
NURU aliishi miaka miatisa na hamsini kasha akafa. “siku zote za Nuru zilikua miaka mia kenda na hamsini, akafa.    (Mwa 9:29)”. Mpango wa shetani wa kuendelea kuwapoteza wana wa Mungu uliendelea.
Vizazi vya wana wa Nuru vilizidi kuzaliana na kuongezeka kadiri siku zilivyokua zikipita. Vilipita yamkini vizazi kadha wa kadha kasha akazaliwa NIMRODI ambaye ndiye tutamzungumzia katika sura hii.”1Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuru, Shemu na Hamu na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika. 2Wana wa Yafethi ni…………  8Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi”    (Mwa. 10:1-8)

NIMRODI alikua mtu aliye jaliwa uhodari wa kupambana na wanyama pori hasa kipindi kile baada ya gharika ambapo walikua wakisumbuliwa na wanyamapori.

Kwakua unabii ulikua unaeleza wazi kuwa atazaliwa MASIHI kwa njia ya wanamke, na kwa njia hiyo ulimwengu wote utaokulewa kupitia kwake, shetani aliamua kuwapotosha watu wa Mungu juu ya mpango mzima wa kuzaliwa kwa MWOKOZI.

Baada ya gharika watu walianza kuhama na kuelekea upande wa mashariki nyanda za chini kuliko na tambarare. Ukanda huu ndi ulikua na ardhi nzuri yenye rutuba iliyokuwa ya udongo wa tifutifu. Udongo huu ulizolewa kutoka sehemu mbalimbali na maji ya Gharika kutoka nyanda za juu.

Watu walianza kuhama na kuelekea katika eneo hili lenye rutuba ili kulima nafaka. Na huko ndiko nchi ya Shinari ilikojengwa.” Mwanzo wa ufalme wake ulikua Babeli na Ereku, na Akadi, na Kane, katika nchi ya Shinari”     (Mwa 10:10).

Shinari ni nchi iliyokua imejaa na kufunikwa na misitu minene, kutokana na udongo wake wenye rutuba hivyo walikua wakishambuliwa mara kwa mara na wanyama pori hatari kama vile Simba, Chui na wanyama wengine.

Ndipo walipotafuta msaada wa mtu yeyote ambaye angeweza kuwaondolea tatizo hilo la kuvamiwa na wanyama pori, na kuahidi kuwa iwapo angepatikana mtu ambaye angewaondolea tatizo lile wangempa heshima kuu.

Alikuwepo mtu mmoja,NIMRODI ambaye alikua hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana, Biblia inamtambua.” 8Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi 9Alikua hodari wa kuwinda wanyama mbele za BWANA. Kwahiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hidari wa kuwinda wanyama mbele za BWANA”(Mwa 10:8,9)

Ndipo walipo msihi sana Nirodi awasaidie kuwaondolea tatizo lile. Nimrodi alifaikiwa kupambana na wale wanyama hatari ka kufanikiwa kulipunguza na kuliondoa tatizo lile. Kwakua tatizo lile lingeweza kurudi tena mda wowote, Nimrodi aliwasihi kujenga mji na kujenga ukuta kuzunguka mji wote. Hivyo ndivyo wangeweza kuwa salama zaidi.

Walifanikiwa kuujenga mji na kujenga ukuta kuzunguka mji wote. Mji huo ukaitwa “MJI WA BABELI”. Kutokana na desturi ya watu wa kale walihitaji kupata mtawala “MFALME” ambaye angewaongeza. Kwa heshima kuu walimsihi Mimrodi awe mfalm wao.

Nimrodi akawa mfale wa kwanza Wa BABELI, na ndiye mfalme wa kwanza kutajwa katika Biblia kuongoza watu baada ya GHARIKA, Biblia inamtambua. .” Mwanzo wa ufalme wake ulikua Babeli na Ereku, na Akadi, na Kane, katika nchi ya Shinari”     (Mwa 10:10).
Hebu turejee vitabu vya kihistoria na maandiko kutoka kwenye biblia,
Mke wa Nimrodi
Jina la Bibi wa Nimrodi ni Ishtar ama Easter. Bibilia yamtaja kama Ashtoreth. Watu wengi walimwita Semiramis na Frazer, (The Golden Bough, ii 275). Njia za hila zake kufanywa kusini mwa Uganda. Jina lingine la Semiramis ni Phrygian Cybele na Assuru Atargati. Jina Atargati ni la kiyunani, kusema Baali ya Tarsus, huko sasani Assuru. Jina lake zamani ilikuwa Atheh-Atheh kumaenisha Mungu mwanamke wa Tarsusi. Mafundisho yake ya uongo ilienea mpaka kaskazini mwa Hieropolis Bambyce karibu na mto Frati (Frazer ibid. v, 162 and n 2,3).
Bwana wake alipokufa, bibi alinyakua mamlaka na kwa sababu watu wengi walikuwa wamepoteza matumaini ya Nimrodi kuwa kama Mungu, kama alivyosema. Seminari aliogopa kupoteza mamlaka yake, na akatafakari hila ya kuondoa ili wamkubali. Hila ya kuwashtua na miuliza ya kufanya waamini kweli Nimrodi alikuwa Mungu.

Baadaye semiramisi akapata mtoto wa kiume, Hii ilikuwa njama na hila ya kudanganya wafuasi wake. Alieneza uvumi ya kwamba mtoto hakuwa na baba, lakini alizaliwa kwa mimjiza kutokana na miale ya jua. Alifahamika kama mtoto wa kurithi ufalme wa Nimrodi.

Huu undanganyifu ulikuwa wa hali ya juu wa kuamini, lakini seminari alifaulu kutawala ufalme. Nimrodi alionekana sana kama motto wa Mungu. Na kwa ajiri ya juhudi zake za undanganyifu seminari aliabudiwa kama ndiye mama wa Mungu. Alijuukana kama “Mama Bikira” au malkia wa mbinguni (Jer 7:18, 44:17-19,25). Ni yeye mama wa kwanza kuwa wa dini ya uongo. Mafundisho ya uongo yaliyomfuata ni ya “Cybele ka mama Mungu huko kati ya mashariki.

Haya yote yametendeka zaidi ya miaka elfu nne iliyopita. Ulikuwa mwanzo wa kuabudu sanamu na imekuwa na uwezo kwa karne nyingi zilizopita, hata siku ya leo, watu wengi wanamwabudu “Malkia wa mbignuni” hata ingawa hakuna mtu kama huyo.



Mfalme Nimrodi akamuoa mke aliyejulikana kwa jina Shemiramisi. Shemiramisi kama malkia wa nchi ile aliishi mdamrefu na mumewe mfalme Nimrodi bila kupata mtoto. Baada ya miaka michache Nimrodi alikufa. Watu wote wa mji ule wa Babeli walihuzunishwa san ana kifo cha mfalme wao NIMRODI.

Baada ya miaka kadhaa kupita, malkia Shemiramisi alipata ujauzito, watu wote walishangaa ni kwa jinsi gani malkia aliweza kuishi na Mfalme Nimrodi bila kupata mtoto. Ili kuficha aibu na kutokuonekana mzinzi, yeye mwenyewe alidai alipata ujauzito kwa njia isiyokua ya kawaida, (KWA NJIA YA MIONZI YA JUA).
Malkia alidai kuwa mfalme Nimrodi alienda kwa Mungu jua na kwa kuwa watu Babeli wanateseka, mfalme nimrodi ameamua kurudi tena kuja kuwaokoa watu wake.

Ghafla ibada za kibabeli zikaanza kufanyika kwa kuangalia jua. Wanadamu walizidi kumchikiza Mungu kwa kufanya mambo ambayo waliyaona ndiyo IBADA ya kweli. 8Akanileta mpaka ua wa ndani ya nyumba ya BWANA, na tazama, mlangoni pa hekalu la BWANA, kati ya ukumbi na madhabahu, walikuwako watu kama ishirini na watano, wamelipa kisogo hekalu la BWANA, na nyuso zao zimeelekea upande wa mashariki, nao wanaliabudu jua”        (Eze 8:16).

Mungu ametuonya kupokea mila za wale wanaoabudu sanamu (Kum. 12:30-31) Viongozi wengi wa kanisa wanatuambia ni ushenzi kutoshika na kuheshimu 25 Decemba kama sikukuu. Hii siku ilisherekewa na washenzi kwa ajili ya kuzaliwa kwa mtoto na malkia wa mbinguni aliyehusishwa na Nimrodi kama Mungu wa jua.
Wafuasi wake wakasema kwa kua tarehe 25th Decemba mti ulinenepa kwa siku moja huko Babeli na Nimrodi angerudi kwa siri tarehe hiyo kila mwaka kuacha zawadi kwa huo mti, aliteremka kama yai kubwa kutoka mbinguni na kuanguka mto frati. Mungu aliyekuja kama yai, si mwingine bali ni ISHTAR. Huo ndio ni mwanzo wa krismasi, Soma karatasi “Kwa nini tusisherehekee krismasi. Why we don’t celebrate Christmas (No. CB24).
Baadaye malkia akaza mtoto akamwita jina lake TAMUZI, Tamuzi alizaliwa tarehe 25 ya mwezi wa kumi na mbili, ambapo siku hiyo kwa heshima ilifanywa ni siku ya amani na msamaha wa wafungwa ulitolewa siku hiyo Biblia inalieleza hilo. 31Hata ikawa, katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake mfalme Yehoyakini, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na tano ya mwezi, Evil-merodaki, mfalme wa Babeli , katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, akamwinua kichwa chake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani.”     (Yeremia 52:31)

Tamuzi alionekana kama mkombozi wao aliyeletwa na Mungu mwenyewe. Uongo dhidi ya ukweli juu ya mpango wa ukombozi wa Ulimwengu kwa njia ya Mwokozi atakayezaliwa na mwanamke ulionekana kama umukwishatimia.

Ghafla ALAMA ZA MOTO kama vile mishumaa ZIKAANZA KUWEKWA KATIKA NYUMBA ZA IBADA  ili KULIENZI JUA(mungu jua) katika siku ambazo jua halijachomoza.

Shemiramisi hakutaka tu aheshimiwe mtoto peke yake, bali pia mama. Baada ya miaka michache kupita mtoto Tamuzi alikufa. Watu wote walisikitishwa sana na kifo cha mungu mtoto TAMUZI.

Watu waliendelea kufanya mambo ambayo yalimchukiza Mungu kama nabii Ezekiel anavyoeleza. ”Akaniambia, mwanadamu, umeyaona haya? Utaona tena machukizo makubwa kuliko hayo.”                         (Eze 8:15)

Baada ya kifo chake Tamuzi, sanamu za kumuenze Tamuzi zikasimamishwa katika nyumba za ibada, Biblia inaeleza. “Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya BWANA, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia Tamuzi”(Eze 8:14)


Tamuzi alikufa katikati ya mwishoni mwa mwezi wa tatu na mwanzonimwa  mwezi wa nne. Baada ya miaka kadhaa kupita malkia shemiramisi naye akafa. Ibada ya mama na mtoto ikaanza kushamiri katika Babeli na Yuda yote. Malkia Shemiramisi kwa hishima akapewa jina la MALKIA WA MBINGUNI.


Ghafla sanamu za ibada ya mama na mtoto zikasimamishwa katika nyumba za ibada. Sanamu hizo zilikua sanamu ya MAMA(Shemiramisi) AKIWA AMEMBEBA MTOTO MIKONONI MWAKE(Tamuzi). Sanamu hizi zilikua zikipewa heshima kubwa katika nyumba za ibada, mashirika mbalimbali ya kinamama yaliundwa na kuamriwa kuamfukuzia uvumba ile sanamu ya malkia wa mbinguni, na kuitunza.

Wakasahau na kuihalifu sheria ya Mungu iliyo kataza sanamu, 1Msifanye sanamu yo yote, wala msijisimamishie sanamu a kuchonga, wala mnara, wala msiweke jiwe lo lote lililochorwa katika nchi yenu ili kulisujudia; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu”    (Kut 26:1)

Kinamama walikua wakiamriwa na waumezao kujiunga katika mashirika na kuiabudu ili sanamu, Biblia inaeleza. 17Lakini bilashaka tutalitimiza kilaneno lililotoka katika vinywa vyetu, kumfukuzia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama tulivyotena sisi na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji wa Yuda……………. Maana wakati huo tulikua na chakula tele, na kufanikiwa, wala hatukuona mabaya”  (Yer 44:17)

Imani zao zilikua kwa miungu na walipoacha kuiabudu, walipatwa na majanga, pomoja na kupungukiwa na chakula. “Lakini tulipoacha kumfukuzia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za vinywaji, tumepungukiwa na vitu vyote; na kuangamizwa kwa upanga na kwa njaa.”  (Yer 44:18)

Kila mume alihakikisha kuwa mke wake amejiunga na shirika ili kuziabudu sanamu zao, na uziunza, Biblia inaeleza vizuri sana.”Nasi tulipomfukuzia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, je! Tulimfanyizia mikate, ili kumwabudu, na kummiminia mamiminiko, waume zetu wasipokuwepo?” (Yer 44:19)

No comments:

Post a Comment