HISTORIA YA MAISHA YA KIKRISTO SEHEMU YA TATU


UNABII KUHUSU BABELI NA HATIMA YAKE
Katika enzi ya manabii wa Israeli (Kama 850-560 K.K) kuliinukia dola mbili kuu katika maeneo yanayoizunguka mito ya Frati na Tigrisi, katika Iraki ya sasa. Ya kwanza ilikuwa dola ya Ashuru iliyokuwa na makao makuu Ninawi.
Kwa karne mbili, Waashuru walivamia  ardhi ya mataifa waliowazunguka: kusini wakawatawala Wakaldayo na makao makuu yake Babeli; na kupitia Israeli mpaka Misri. Sera yao ilikuwa kuwatishawakazi wa maeneo hayo watii na kulipa kodi kwa mwaka. Kufanikisha hili waliiswaga miji kiuporaji na kuichoma moto, wakavibamiza vijiji, na kuua wakazi na kuchukua maelfu ya mateka Ashuru.
Katika nusu ya pili ya karne ya saba (K.K), nguvu ya Ashuru ilipungua na Babeli ikaanza kupanda. Katika mwaka  612 (K.K), Ninawi uliangushwa. Nebukadreza, mfalme wa Wakaldayo, haraka akaanzisha dola mpya.
Mataifa madogo madogo Mashariki ya Kati yalipokuwa yanashangilia uhuru wao kutoka Ashuru, mara yakajikuta wakivamiwa na majeshi ya Babeli. Nebukadreza akaivami Israeli akaiteka Yerusalemu, akalichoma hekalu  lake na kuchukua maelfu ya mateka Babeli.

Dola ya Babeli ilikuwa ni  awamu ya pili ya utawala huu wa kijeshi. Ulikuwa katika eneo la Frati. Nebukadreza, aliujenga mji mkuu wa Babeli kuwa fahari ya dunia. Alijenga Mahekalu makubwa na majumba ya kifalme, na kuzungushia jiji hilo ukuta mkubwa sana kuulinda. Babeli ukawa utukufu na fahari kuu kwa Nebukadreza mwenyewe na Wakaldayo wake.

MAANGUKO KAMILI
Miaka 100 kabla Babeli haijafikia kilele cha ukuu wake, nabii Isaya alishatabiria kuangushwa kwake kwa maneno thabiti sana. “…Siku ya BWANA i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu…Tazama, nitawaamsha Wamedi juu yao…Na Babeli, huo utukufu wa  falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama  Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza. Hautakaliwa na watu tena kabisa… Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani”    (Isaya 13:6,17,19-21).
Nabii mwingine, Yeremia, akiandika miaka 100 baadaye, wakati Nebukadreza alipokuwa akikaribia kuivamia Yerusalemu, aliongeza mtazamo juu ya anguko la Babeli. Na mwishowe nabii anaamriwa kufunga jiwe kwenye gombo la unabii ule na kulitupia ndani ya mto Frati, aseme, “Hivyo ndivyo utakavyozama Babeli, wala hautazuka tena…
Soma kifungu cha   (Yer:51:1,8,28,37,58,62-64).

Historia inaonyesha jinsi ambavyo unabii huo wa maanguko ya Babeli ulivyotimizwa hatua kwa hatua. Wavunjaji  wa Kwanza walikuwa Wamedi na  Wajemi katika karne ya sita (K.K). Baadaye walikuja Wayunani chini ya Aleksanda Mkuu, wakifuatiwa na Warumi; baada yao makabila kadhaa yapendayo vita kama Wapathi, Waarabu na Watarta.

Kwa karne nyingi mahali halisi pa jiji la Kale la Babeli palikuwa mahame, yaliyoepukwa -wasafiri wasemavyo -na  wahamaji wanaotangatanga. Ni hivi karibuni tu wataalamu wa kihistoria wachimbuao chini (Archaeologists), walipochunguza eneo hilo katika nusu ya kwanza ya karne ya 19, na kugundua mabaki ya kuta kubwa, mahekalu ya  nguvu na malango, na masanamu makubwa yaliyoonyesha ulimwengu ulioshikwa na butwaa jinsi ukuu wa Babeli ulivyokuwa enzi zake.
Kwa hiyo historia inatuonyesha jinsi Babeli ‘Utukufu wa falme,’ ulivyoangushwa na kuachwa, kama manabii wa Israeli walivyotabiri ingekuwa.

Nani angeweza kujua?
Utabiri wa mambo wa muda mrefu hivyo unawezekanaje? Kuna jibu moja tu linaloridhisha; Lazima awep aliyeyajua kabla; lakini ni nani? Kwa hakika hakuna mtu wa miaka 2500 iliyopita au tangu hapo, angeweza kujua.
Tukiupima utabiri wa namna hii kibinadamu tu hauelezeki. Lakini hata hivyo, manabii wa Agano la Kale hawakudai wanatabiri kwa uwezo wao. Walisema walikuwa wakisema  manena yaliyotoka kwa Mungu. “ Hivi ndivyo asemavyo BWANA,” ndivyo walivyokuwa wakianza kusema wakati wote.
Kama Mungu alikuwa nyuma ya yale waliyosema, tunapata jibu la nani aliyejua.’ Hakuna maelezo mengine yanayoleta maana. Unabii tuliouchunguza hapa ulihitaji uwepo wa Mungu kama chanzo chake

No comments:

Post a Comment